Chuma Blog
CHUMA BLOG inampa pole Sauda Mwilima kwa kupoteza mtoto.

Mtangazaji wa kipindi cha Bongo Beats cha Star TV amefiwa na
mtoto wake wa kiume muda mfupi baada ya kujifungua.
Kwa mujibu wa website ya Diamond, Sauda alijifungua mtoto huyo juzi kuamkia jana katika hospitali ya
Kinondoni kwa Doctor Mvungi lakini wa bahati mbaya mtoto wake alifariki dunia.
Hata hivyo mtandao huo umedai kuwa Sauda bado yupo hospitali na afya yake
inaendelea vizuri.
Mwezi April mwaka huu, mtangazaji huyo alifunga pingu za
maisha na Kauli Juma, katika harusi iliyohudhuriwa na mastaa.
No comments:
Post a Comment