Friday, March 30, 2012

"Beatrice" Atokwa na machozi studio......................

Chuma Blog

Dyna, Beatrice, Rachel & Queen.
Katika kipindi cha Diva Loveness Love wa ALA ZA ROHO Clouds fm... live kwenye show yake alhamis march 29 usiku... huwa kila alhamis moja katika mwezi mmoja show yake ya radio inaungana na Clouds Tv, wasanii wanaalikwa na kuimba Live pamoja na mahojiano.
Waliimba live na kuhojiwa! Beatrice alitokwa na machozi wakati akizungumzia alikotoka na alipo sasa.Kwani alifunguka na kusema, kazi wanazofanya wasanii wengi wa kitanzania,jinsi wanavyochukuliwa  kimataifa  ni tofauti  sana  na  maisha  yao  halisia yao.Alisema kwa  mfano  mimi  simu  ninazopigiwa  toka  kenya,  burundi  nk  naonekana  ni msanii  mwenye  mafanikio.Kwani mwaka wote nimefanya show kubwa mbili tu hadi sana.Ila inatia uchungu  kwa  kweli,nawaomba wadau  waangalie maslahi  yetu,kwani tunateseka  sana" Alisema  Beatrice  huku  akilia  kwa  uchungu. Kwa  upande  wake  msanii  Dareen  alionekana  kukazia  hoja  hiyo  huku  akielekeza  kilio  chake  serikalini.
     Wasanii  hao  wakike  ambao  ni  nominees  wa  KILI MUSIC  AWARD  walitoa  malalamiko  hayo   walipoitwa  katika  studio  za  clouds fm  katika  kipindi  cha  Ala  za  Roho kinachoendeshwa  na mtangazazi loveness  love,  pia  kilirushwa  live  na  kituo  cha  clouds tv  na  kuwapa  nafasi  ya  wasanii  hao  kuomba  kura kwa  mashabiki  ili  wawachague  katika  mashindano  ya  kili music  award   2011-2012.

No comments:

Post a Comment