Thursday, June 14, 2012

SAM WA UKWELI SIJAFURIA ....

 
Baada ya ukimya wa muda mrefu  hatimaye  mkali kutoka gemu ya muziki wa Kizazi kipya Bongo  Salum Mohamed  ‘Sam wa Ukweli’ anatarajia kutoka na albamu mpya aliyoibatiza jina la ‘ Hisia Zangu’.


Sam  amefunguka kuwa  ukimya uliokuwepo ulitokana na  kubanwa na majukumu ya kifamilia  na ukosefu wa menejimenti wakati alipokuwa  akitoka  kwa mara ya kwanza .
“Ulikuwa  ni wakati mgumu  kwangu kwa sababu sikuwa na menejimenti wakati ninatoka mara ya kwanza  hivyo nilijikuta kwenye majukumu mengi  hasa baada ya kuoa,  hata hivyo nashukuru  kuwa nimepeta menejimenti  na tayari niko kwenye harakati za  kugonga ‘kichupa  kipya’  tayari kwa mtoko wa  albamu yangu niliyoibatiza  jina la  ‘Hisia zangu’ na singo ya kwanza  kutoka  itakuwa ni ‘Najua’ ambayo ndani yake  nimejaribu kuzungumza juu ya wale wanaodhani kuwa  bila wao mambo mengine  hayaendi” alisema Sam wa  Ukweli
 Katika hatua nyingine Sam amedokeza kuwa  hakuna ukweli wa aina yoyote juu  ya tetesi  zilizoenea mtaani kuwa amefulia kimuziki , huku pia akitupilia mbali tetesi kua alichanua  kwenye gemu kwa kuwa alikuwa akitungiwa mashairi.
 “Mimi sijawahi kutungiwa mashairi , na siyo kweli  kwamba nimefulia  ni mipango tu  lakini  napenda kusema kuwa  huu  ni wakati wangu wa kuwaziba midomo  waliokuwa wakinishambulia”  alisema  Sam.

No comments:

Post a Comment