Monday, January 16, 2012

TETEMESHA WASHUKURU WADAU KWA KUPOKEA VIZURI KAZI ZA WASANII WAO

Sisi kama TETEMESHA RECORDZ tumejiwekea malengo ya kuwa tunajaribu kutafuta wasanii wachanga kabisa lakini wenye vipaji na kuwapika kisha kuwatambulisha katika music industry hapa TZ.Tulianza na HUSSEIN MACHOZI, akafuata SAJNA na sasa ni zamu ya msanii mwingine mpya C-SIR MADINI kutoka Mwanza Na sasa tumeshamtambulisha kwenu PETER MPONEJA, na jina lake lingine la nyumbani ni MASISA, hilo MASISA lilikuwa jina la babu yake, na kutoka katika hilo ndio akaamua kulifupisha kuwa SISA na ndilo anatumia katika muziki lakini katika matumizi ya Muziki litakuwa likiandikwa C-SIR.Katika wimbo wake wa kwanza ambao umeshaanza kupata mafanikio makubwa tunajiandaa kukamilisha album yake ya kwanza ambayo bado tunaendelea kuirekodi. Video ya wimbo huu imekwishafanyika chini ya ADAM JUMA wa NEXT LEVEL ambayo mpaka sasa imepokelewa vyema.Tunakurukuru sana mdau kwa kupokea kazi zetu...

No comments:

Post a Comment