Sunday, January 29, 2012

SITAKI TENA KUTEMBEA NA MASHAROBARO WEMA SEPETU…!!

BAADA ya matatizo ya mapenzi, hatimaye msanii Wema Sepetu, ameweka wazi kuwa hataki tena kutembea na masharobaro kwani mapenzi yao yanakuwa hayana malengo zaidi ya kuchezeana.
Akizungumza hivi karibuni msanii huyu alisema kuwa msanii anayemfananisha na sharobaro ni aliyekuwa mpenzi wake Nassib Abdul ‘Diamond’, kwani endapo angekuwa hayuko hivyo basi anaamini mapenzi yao yangedumu kwa muda mrefu.
Alisema kwa sasa anahitaji kutoka na mwanaume aliyemzidi umri kwani anaamini watu hao wanakuwa na mapenzi ya dhati tena hawana wivu kama watoto wadogo ambao muda wote hupenda kuwa karibu na wapenzi wao badala ya kufanya kazi.


“Kila kitu kina muelekeo wake, mapenzi yangu mimi na Diamond yangeweza kudumu lakini kutokana na usharobaro alionao ndiyo uliosababisha yote yaliyotokea, na ndiyo maana nasema kwamba ni bora kutembea na mwanaume aliyekuzidi umri mnaweza kufika mbali,” alisema.
Msanii huyu alisema hata hivyo ni bora afunge ndoa na mwanaume atakayempata ambaye anajua maana ya mapenzi kuliko kutembea na vijana wadogo ambao hawajui nini maana ya mapenzi na hawana muelekeo wa maisha.

2 comments:

  1. hata mimi nakuunga mkono,usirudi tena kwa diamond
    hakufai huyo,anakupotezea mda bure,ukirudi tu atakufanyia vituko kuliko hivyo,atakuona huwezi kumkosa,wewe bado unaita,hujazeeka wema,hajui maana ya penzi.please please please usirudi.

    ReplyDelete
  2. nyimbo yake nimpende nani.JOKATE AU WEMA,na sifa nyingi ni za kumsifu JOKATE,inaonesha wazi walikuwa na uhusiano wa mapenzi,sasa anageuza kibao,ati WEMA ni ubavu wake na Jokate ni dada ake.Muongo huyo wanaficha aibu yao,na kuandikwa magazetini.achana naye hiyo sharobaroooooo.I LOVE YOU SO MUCH,sister WEMA.Tulia utapa mchumba ,mwenye kheri na wewe ok

    ReplyDelete