Chuma Blog

Nyota wa muziki wa kizazi kipya Bongo, ALLY Timbulo ‘Timbulo’ amepatwa na tukio la aina yake baada ya wajanja wa Bush kumliza kamera kubwa aina ya sonny wakati wa paty maalumu aliyoifanya mwishoni mwa wiki iliyopita kijijini kwao Riuwa, Wilayani Mbalali jijini Mbeya.
Akizunguma na Teentz mapema leo Timbulo amesema kuwa aligundua kupotea ghafla kwa kamera yake hiyo mara baada ya kumalizika kwa paty hiyo iliyokuwa imechangamka kupita kiasi huku vijana wengi aliokuwa wamefurika wakiwa hoi kwa mitungi.
“Nilipomaliza kuimba nikawa nimechili sehemu napumzika, lakini baada ya party kuisha nianza kukusanya vitu vyangu na baadae nikagundua kuwa kamera yangu haipo, kwa kweli nilichanganyikiwa kwa kuwa bado ni mpya kabisa na niliinunua kiasi cha dola 800 za Marekani” alisema Timbulo
Akiendelea zaidi timbulo amesema kuwa juhudi za kumsaka mtu aliyesepa na kamera hiyo ya kisa bado zinaendelea kwa kuwa sehemu kubwa ya watu waliofika siku hiyo wanafahamiana hivyo anaamini ndani ya siku chache zijazo atakuwa ameipata.
katika shoo hiyo Timbulo amerifu kuwa jukwaa alilokuwa analitumia kuwaburudisha mashabiki wake lilishindwa kuhimili vishondo na kuvunjika kufuatia watu kushindwa kuvumilia na kupanda juu alipokuwa yeye na hatimaye jukwaa hilo likasalimu amri.
“Hakika ilikuwa siku mbaya kwani kuna mambo mengi yalijitokeza ikiwamo shughuli yangu kucheleweshwa baada ya mchana na kuwa ucku kutokana na mtendaji wa kata kuzuia mpaka diwani alipoingilia kati na kuniruhusu” alimaliza.
STORI NA: DISMAS
Nyota wa muziki wa kizazi kipya Bongo, ALLY Timbulo ‘Timbulo’ amepatwa na tukio la aina yake baada ya wajanja wa Bush kumliza kamera kubwa aina ya sonny wakati wa paty maalumu aliyoifanya mwishoni mwa wiki iliyopita kijijini kwao Riuwa, Wilayani Mbalali jijini Mbeya.
Akizunguma na Teentz mapema leo Timbulo amesema kuwa aligundua kupotea ghafla kwa kamera yake hiyo mara baada ya kumalizika kwa paty hiyo iliyokuwa imechangamka kupita kiasi huku vijana wengi aliokuwa wamefurika wakiwa hoi kwa mitungi.
“Nilipomaliza kuimba nikawa nimechili sehemu napumzika, lakini baada ya party kuisha nianza kukusanya vitu vyangu na baadae nikagundua kuwa kamera yangu haipo, kwa kweli nilichanganyikiwa kwa kuwa bado ni mpya kabisa na niliinunua kiasi cha dola 800 za Marekani” alisema Timbulo
Akiendelea zaidi timbulo amesema kuwa juhudi za kumsaka mtu aliyesepa na kamera hiyo ya kisa bado zinaendelea kwa kuwa sehemu kubwa ya watu waliofika siku hiyo wanafahamiana hivyo anaamini ndani ya siku chache zijazo atakuwa ameipata.
katika shoo hiyo Timbulo amerifu kuwa jukwaa alilokuwa analitumia kuwaburudisha mashabiki wake lilishindwa kuhimili vishondo na kuvunjika kufuatia watu kushindwa kuvumilia na kupanda juu alipokuwa yeye na hatimaye jukwaa hilo likasalimu amri.
“Hakika ilikuwa siku mbaya kwani kuna mambo mengi yalijitokeza ikiwamo shughuli yangu kucheleweshwa baada ya mchana na kuwa ucku kutokana na mtendaji wa kata kuzuia mpaka diwani alipoingilia kati na kuniruhusu” alimaliza.
STORI NA: DISMAS
No comments:
Post a Comment